![]() |
| Baadhi ya wanachama wa SACCOS ya walimu Songea mjini |
Na Albano
Midelo
MKUU wa wilaya ya
Songea Joseph Joseph Mkirikiti ametahadharisha kuwa vyama vingi vya kuweka na kukopa (SACCOS)
vinavunjika kutokana na uongozi mbovu ambao unashindwa kuwahudumia wanachama
wake kulingana na katiba yake.
Mkirikiti alitoa
tahadhari hiyo wakati anafungua mkutano mkuu wa 15 wa chama cha ushirika wa
akiba na mikopo cha walimu wa manispaa ya Songea ambao ulifanyika kwenye ukumbi
wa Songea klabu.
‘‘Uongozi mbovu ambao
unashindwa kuwahudumia wanachama wake unasababisha wanachama wake kukosa raha
na kupooza hali ambayo inaweza kusababisha saccos kutoweka, baadhi ya viongozi katika saccos wanakosa maono hivyo
wanafanyakazi kwa upendeleo na ubaguzi jambo ambalo ni hatari katika ushirika’’,alisisitiza.
| Mwenyekiti mstaafu Saccos ya walimu wa Songea mjini Martin Challe |
Mkirikiti ambaye kabla
ya kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa
mkuu wa wilaya ya Songea alikuwa ni meneja wa saccos jijini Dar es salaam
ametoa wito kwa viongozi wote wa saccos kujipanga upya ili saccos wanazoziongoza ziwe
na nguvu kubwa kiuchumi ili kumudu
ushindani dhidi ya vyombo vingine vya fedha.
‘‘Hivi sasa kuna
wimbi kubwa la wanachama ambao wanajitoa uanachama katika saccos ,viongozi wa
saccos hakikisheni wanachama wote ambao
wanajitoa uanachama wanaelimishwa ili wasiendelee kujitoa vinginevyo siku moja saccos inaweza kutoweka na mimi
kama mtu mwenye taaluma ya ushirika siwezi kukubali hili liendelee kutokea ni aibu
kwangu’’,alisema.
Kwa upande wake
mwenyekiti wa saccos hiyo Martin Challe alizitaja changamoto ambazo
zinakikabili chama hicho kuwa ni pamoja na ushirikiano mdogo toka kwa baadhi ya
wanachama, hazina kuingiza makato pungufu ya mikopo kutokana na uwezo mdogo wa
mishahara ya wakopaji na wanachama 20 walijitoa katika kipindi cha kuanzia
Januari hadi Desemba 2012 kutokana na sababu mbalimbali.
Mwenyekiti huyo
ambaye ameiongoza saccos ya walimu kwa miaka 15 katika mkutano mkuu huo
alijitoa kwenye kamati ya wajumbe wa
Bodi ya saccos hiyo hivyo kupoteza nafasi yake ambayo sasa imechukuliwa na
mwenyekiti mpya wa saccos ya walimu Gosbert Nchimbi.
Risala iliyosomwa na
makamu mwenyekiti wa saccos hiyo Julia Luoga inaonyesha kuwa saccos ina akiba
za wanachama zaidi ya sh.milioni 490,mikopo iliyotolewa na wanachama ni zaidi
ya sh.milioni 357,Hisa zaidi ya milioni
36 na Amana ni zaidi ya milioni moja.
Baadhi ya wanachama
wa saccos hiyo wakiwemo Ajaba Chitete,Stefano Haule na Thomas Kongo wameelezea
athari za wanachama kujitoa katika saccos
kunasababisha riba na akiba
nyingi za wanachama waliojitoa kupotea na kwamba nguvu ya vyama vya
akiba na mikopo ni uwingi wa wanachama.
Wamedai kuwa Kasi ya wanachama kujitoe katika
saccos ya walimu kila mwaka inakiweka chama hicho mashakani,na kwamba saccos
hiyo hivi sasa ni dhaifu sana
ukilinganisha na saccos nyingine wilayani Songea ambazo zimeanzishwa karibuni
,hivyo wamewaomba viongozi waliopo wabadilike kifkra na kimtazamo ili kuikoa
saccos hiyo ambayo ilikuwa mfano wa kuigwa.
‘‘Saccos hii ni yetu
ni lazima tujiulize kwanini idadi kubwa ya wanachama wanajitoa ,hapa kuna
tatizo kubwa,mwanachama anahitaji mkopo wa shilingi milioni nne chama kinampa shilingi laki mbili
hali ambayo inamfanya mwanachama kushindwa kutumiza malengo yake’’,alisema
Chitete.
Wanachama hao pia
wamedai uongozi uliopo madarakani umeshindwa kusimamia ujenzi wa mradi wa jengo lao ambao walidai unatia
mashaka kutokana na mradi huo kutumia muda mrefu na fedha nyingi za wanachama zinaendelea kutumika bila mradi
wa kitega uchumi kukamilika.
“Tunamwomba mwenyekiti wetu atoe
taarifa ya ujenzi wa jengo hili kwa sababu hadi sasa hatujui fedha kiasi gani
zimetumika kwenye mradi huo na bado shilingi ngapi kukamilisha ujenzi,kwanini
uongozi uliamua kumtumia mkandarasi ambaye anatupa mashaka kwa kuwa ujenzi wake
haukamiliki licha ya kutumia fedha nyingi na muda mrefu’’,alihoji mwanachama
Ajaba Chitete.
Mwenyekiti wa saccos hiyo aliyejitoa kwenye
Bodi Martin Challe katika mkutano mkuu
wa 13 alisema hadi kufikia mwaka 2009 zaidi ya sh.milioni 138 zilitumika katika
ujenzi wa kitega uchumi cha walimu na
kwamba kitega uchumi hicho kinatarajia kugharimu sh. milioni 198 hadi kitakapokamilika.
Chama cha ushirika wa akiba na mikopo cha walimu wa
manispaa ya Songea chenye wanachama 375 kati yao wanaume 107 wanawake 266 na
Taasisi mbili kilianzishwa rasmi Septemba 1998.
CHAMA kimoja cha
ushirika wa akiba na mikopo wilayani Mbinga mkoani Ruvuma mwaka 2009 kilidaiwa kusambaratika
kufuatia upotevu wa shilingi milioni 400
ambazo hazikufahamika nani wa kumkata
hali iliyowasababisha wanachama kuwataka viongozi wake kuwajibika na sheria
kuchukua mkondo wake.
albano.midelo@gmail.com,simu
0766463129

No comments:
Post a Comment