Maendeleo ni Vita
Pages
Makala za uchunguzi
Makala za utalii
Makala za Elimu
Makala za mazingira
Makala za kijamii
Habari katika picha
Sunday, October 2, 2011
Umwagaji wa sumu katika mto Lunyere unaanzia nchini Msumbiji
Hapa ni kitongoji cha Songeapori kilichopo mpakani na nchi ya Msumbiji ambapo wachimbaji wadogo wadogo akiwa mmoja mmoja wanatumia zebaki kusafishia udongo wenye dhahabu na kusababisha uchafuzi wa maji ya mto huo ambao unategemewa na viumbehai akiwemo binadamu wilayani Mbinga.Mto huo unaingia katika pori la wanyama la Liparamba ,kuungana na mto Ruvuma kisha kumwaga maji yake katika Bahari ya Hindi.Wataalamu baada ya kuyapima maji ya mto huo wamesema maji hayo hayafai kwa matumizi ya binadamu na viumbe hai kutokana na viwango vya sumu kupita vinavyokubalika kitaifa na kimataifa picha na maelezo na Albano Midelo
Picha hii imepigwa katika kijiji cha Mpapa Lupilichi mkoa wa Lichinga,milima inayoitwa Sufuri A ndiyo chanzo cha mto Lunyere ambapo wachimbaji wa madini wamekuwa wanatumia vyanzo hivyo vya maji kusafishia udongo wenye dhahabu kwa kutumia zebaki na kusababisha uchafuzi hivyo kuathiri viumbe hai katika nchi ya Tanzania ambako mto huo unapita na kuungana na mto Ruvuma kisha kumwaga maji yake Bahari ya Hindi maelezo na picha kwa hisani ya Albano Midelo.
No comments:
Post a Comment
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment