Tuesday, May 8, 2012

Barua ya wazi kwa Rais Mkapa

MIMI ni mwalimu mstaafu John Joseph Haule ambaye ninaishi Songea mjini, nilizaliwa Aprili 6,1936,nilikuwa  mwalimu wa shule ya msingi Lupaso,Migongo na Makanya wilayani Masasi mkoa wa Mtwara katika kipindi cha mwaka 1959 hadi 1966.


Kabla ya kustaafu kazi mwaka1992 nimewahi kufanyakazi katika wizara ya elimu kama mwalimu katika shule mbalimbali,mratibu elimu,mkuu wa chuo cha maendeleo ya wananchi na mkaguzi wa shule.
Namba yangu ya pensheni ni 0036642 na TYR 125586.Hata hivyo pensheni yangu ya Julai hadi Desemba 2011 ambayo ni jumla ya shilingi  laki tatu(300,000) haijalipwa kwangu hadi leo licha ya kuandika barua kadhaa kupitia ofisi ya hazina ndogo mkoa wa Ruvuma bila mafanikio.
Inadaiwa jina langu linafanana na mstaafu mwingine wa kule wilayani Mbinga mkoani Ruvuma ambaye anaitwa  John Mhanga Haule hata hivyo namba zetu na sura zetu ni tofauti kabisa.
 Mheshimiwa Rais mstaafu,nikiwa katika shule  za wilayani Masasi wakati huo miongoni mwa washauri wangu wakuu ni pamoja na baba yako mzazi hayati William Mkapa,padre Philipo Mrope,Kilian Namajojo na Mwenyi John Mkonona aliyesimamia ubatizo wa mtoto wetu wa kwanza aliyezaliwa katika zahanati ya Lupaso.
Kwa upendo na heshima uliokuwa nayo kwa wazee wa pale Lupaso wakiwemo hao ambao nimewataja hapo juu,nakuomba tafadhali unisaidie ili niweze kupata fedha yangu hiyo kwa kuwa nasumbuliwa mno na magonjwa sugu ya kisukari,BP,ubovu wa macho na matatizo mengine ya uzeeni.
Sina cha kukupa ,mwenyezi Mungu akubariki ni mimi John Haule wa SLP 128  Songea,simu 0684804290 AU 0714089538.

No comments:

Post a Comment