Saturday, January 26, 2013

Mwalimu anaishi maisha ya enzi za ujima ni aibu

Mmoja wa walimu katika shule ya msingi Liwundi wilayani Nyasa mkoani Ruvuma akiwa amekaa chini ya nyumba yake ambayo kwa mujibu wa maelezo ya mwalimu huyo nyumba hiyo wakati wa mvua za masika inavuja na kusababisha mwalimu pamoja na familia yake kupata usumbufu ikiwemo kusimama wima kutokana na nyumba kugeuka bwawa,Aidha vitu vyake vya ndani zikiwemo samani na maandalio ya masomo yanaharibika baada ya kulowa na maji.Maelezo na picha na Albano Midelo

Hapa ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi Liwundi akionyesha choo ambacho anatumia mwalimu katika shule hiyo ambacho mazingira yake yanakatisha tamaa hali ambayo inasababisha walimu wanaopangiwa katika shule hiyo kukataa kuripoti na wanaoripoti hufundisha kwa muda mfupi kisha kuomba uhamisho au kuacha kazi.

Hapa ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ngumbo wilayani Nyasa mkoani Ruvuma akimwonyesha mwandishi  nyumba ya mwalimu ambapo walimu wengine katika shule hiyo hawana kabisa nyumba,Hali hii inasababisha walimu wengi kukata tamaa na kuona kuwa kazi ya ualimu ni adhabu na haina thamani,hii ni changamoto kwa wadau wote wa elimu kubadilika kifkra na kimtazamo ili walimu waonekane kuwa ni watu muhimu katika nchi hii vinginevyo hata elimu ikitolewa bure kuanzia shule ya msingi hadi sekondari kama walimu hawatathaminiwa ni kazi bure


Hili ndilo jiko ambalo anatumia mwalimu katika shule ya msingi Liwundi wilayani Nyasa mkoani Ruvuma,mkewa wake anamwandalia chakula hapa mme wake ambaye anafundisha katika shule hiyo.Hii ni aibu hebu tubadilike walimu waishi katika mazingira ambayo yanalingana na wakati tuliona nao ili watoe elimu bora na sio bora elimu.Maelezo yote na picha na Albano Midelo

No comments:

Post a Comment