![]() |
| Viongozi na wajumbe wa kamati ya utendaji ya TAMH mkoa wa Ruvuma |
Na Albano
Midelo
VIONGOZI na wajumbe wa kamati ya utendaji 15 wa chama
cha watu wenye ulemavu wa akili (TAMH) mkoani Ruvuma wamepata mafunzo ya
siku tano ya kuandaa mpango mkakati,usimamizi wa fedha na rasilimali watu.
Mafunzo hayo ambayo yamefanyika
kwenye ukumbi wa maktaba mkoa wa Ruvuma yaliofadhiliwa na shirika lisilo la
kiserikali la The Foundation For Civil Society
yameshilikisha wajumbe kutoka Halmashauri za Songea manispaa,Namtumbo na
Songea vijijini.
Mwenyekiti wa TAMH
mkoa wa Ruvuma Thadei Mwakaguo alibainisha kuwa shirika la The Foundation For
Civil Society limetoa shilingi milioni 7.5 kwa chama hicho kwa lengo la wajumbe
wa kamati ya utendaji katika mkoa mzima kuendesha mafunzo ya mpango mkakati
,usimamizi wa fedha na rasilimali watu.
‘‘Wafadhili baada ya
kukubali kutupatia kiasi hicho cha fedha walitoa maelekezo namna ya kutumia
fedha hizo ambayo ni kuandaa mpango mkakati wa chama,kuendesha mafunzo ya usimamizi wa fedha,mafunzo ya katiba kwa
wanachama ambao ni wenye ulemavu wa akili na kufanyika mdahalo wa wazi ambao
utakusanya mawazo ya wenye ulemavu ambayo yatatumwa katika kamati ya kukusanya
maoni ya katiba’’,alisisitiza.
Mgeni rasmi katika
ufunguzi wa mafunzo hayo afisa ustawi wa jamii mkoa wa Ruvuma Anna Mwingira
pamoja na mambo mengine aliikumbusha jamii kuachana na mila potofu kuhusu watu
wenye ulemavu badala yake sasa kubadilika na kuwashirikisha wenye ulemavu
katika mambo mbalim bali kwa kuwa wana nafasi ya kuchangia katika ujenzi wa
Taifa.
Wawezeshaji katika mafunzo hayo ni Victory Nyenza afisa ustawi wa jamii
katika manispaa ya Songea na Mussa Ndomba mkurugenzi wa shirila lisilo la kiserikali la
LESCOTA ambalo linashughulikia masuala
ya watoto waishio katika mazingira hatarishi.
albano.midelo@gmail.com,simu 0766463129

No comments:
Post a Comment