![]() |
| Brighton Mwandata mwanamuziki wa injili TAG Songea |
Na Albano Midelo
MWANAMUZIKI anayeibukia
kwa kasi katika muziki wa injili Brighton Mwandata wa mjini Songea baada ya
kuzindua albamu yake ya kwanza ya (UTUSAIDIE YESU) ameanza ziara nje ya nchi na
mikoa mbalimbali hapa nchini.
Mwandata hivi
karibuni ametumbuiza katika mkutano mkubwa wa injili jijini Lusaka nchini
Zambia akishirikiana na waimbaji maarufu wa muziki wa injili ambao ni Abiudi
Misholi,Daniel Mboya na Martha Baraka.
Wimbo wake wa Nasikia
kuitwa aliyoimba kwa lugha ya kabila la Kisafwa la mkoani Mbeya
umewavutia wananchi wengi nchini Zambia ambao waligombania albamu hiyo na kuacha gumzo kubwa katika nchi hiyo.
umewavutia wananchi wengi nchini Zambia ambao waligombania albamu hiyo na kuacha gumzo kubwa katika nchi hiyo.
Akizungumza katika
mahojiano maalum na mwandishi wa makala haya Mwandata alisema katika mkutano
huo aliweza kuimba nyimbo zake karibu zote za albamu yake ya audio na video iliyobeba jina la Utusaidie yesu
ikiwa na nyimbo nane ilirekodiwa katika studio za Paradise na G&J
production mjini hapa kati ya mwezi Machi na Desemba mwaka jana tayari imekamilika
.
![]() |
| Mke wa mwanamuziki Mwandata ambaye pia ni mwimbaji |
Uzinduzi rasmi wa
albamu hiyo ulifanyika katika kanisa la TAG Misufini Songea Julai 21 mwaka huu,
mgeni rasmi alikuwa ni mwanasiasa maarufu wa mjini Songea Paulo
Mtewele(Mbogolo) ambapo jumla ya shilingi milioni saba zilipatikana.
‘‘Audio na video zimenigharimu
karibu shilingi milioni sita,nyimbo zilizopo katika albamu yangu ni simama, usicheze
na wokovu, utusaidie Yesu,watashindana,wewe ni baba,nasikia kuitwa na hakuna
kama Yesu,katika huduma ya uimbaji hakuna mtu yeyote ambaye ananisaidia iwapo yeyote
ameguswa na huduma hii anaweza kunisaidia ilikufikia malengo katika
uimbaji’’,alisisitiza.
Mikoa mingine
ambayo amebahatika kutumbuiza na
kuitangaza albamu yake ni pamoja na Dar es salaam Morogoro, Mbeya,Pwani,Dodoma na Njombe na
hivi karibuni anatarajia kwenda katika mikoa mingine ya hapa nchini pamoja na
nchi ya Kongo DRC.
Mwandata ambaye
kitaaluma ni fundi wa vifaa vya umeme alijiingiza katika uimbaji wa nyimbo za
injili tangu mwaka 2004 ambapo alijiunga na kwaya ya Soul Winners ya kanisa la
TAG Misufini mjini hapa ambayo anaendelea kuimba hadi sasa.
Mwandata hivi sasa amejiajiri mwenyewe,awali alikuwa
anafanyakazi katika shirika la viwanda vidogo SIDO na kampuni ya Songea Cable Television kabla
ya mwaka jana kuacha kazi na kujiajiri yeye mwenyewe ambapo muda wake mwingi anautumia kwa ajili
ya kumtumikia mwenyezi Mungu kwa njia ya uimbaji.
Iwapo unataka
kuwasiliana na mwanamuziki huyu unaweza kutumia simu +255753397336 AU
+255714917461 BARUAPEPE brighton.mwandata@gmail.com


No comments:
Post a Comment