Na Albano Midelo
Wanachuo katika chuo
kikuu cha mtakatifu Joseph tawi la Songea wanadai kubaguliwa na kunyanyaswa na
baadhi ya wahadhiri raia wa India katika chuo hicho ni moja ya sababu
zilizowafanya kufanya mgomo kushinikiza uongozi wa chuo kupatia ufumbuzi madai
yao.
wametoa madai
mbalimbali ya muda mrefu yaliosababisha kufanya mgomo na vurugu kwa kuwa
uongozi wa chuo umeshindwa kuyapatia ufumbuzi hadi sasa.
Wakizungumza huku
wakikataa majina yao kuandikwa kuhofia kufukuzwa chuo,waliyataja baadhi ya
madai hayo kuwa ni kunyanyaswa na uongozi kwa kukatazwa kuingia chuoni hapo
na vifaa muhimu vya mawasiliano ikiwemo
simu na kompyuta ndogo yaani latop.
“Dean of student
akikukamata na simu au laptop anakunyang’anya na unarudishiwa vifaa vyako baada
ya semester kumalizika kwa kweli tunanyanyaswa sana kufanyiwa mambo haya
wanachuo wa chuo kikuu,tunaomba Tume ya vyuo vikuu kuingilia kati suala hili
sisi sio wanafunzi wa sekondari’’,alidai mmoja wa wanachuo.
Madai mengine ambayo yalisababisha
waandamane na kugoma kuingia madarasani kuwa ni kushinikiza Rais wa serikali ya
wanachuo Aristides Mujwahuzi pamoja na waziri wake mkuu Deogratias Sanga ambao
walivuliwa nyazifa zao na kusimamishwa masomo kwa muda wa miezi sita,warudishwe
na waendelea madaraka yao.
Kulingana na wanachuo
hao madai mengine ni chuo hakina mazingira bora ya kusomea na vyoo vilivyopo
ndani ya eneo hilo ni vichache ambavyo havina hadhi ,pia kuna uhaba mkubwa wa
maji jambo ambalo limekuwa liwasababishia kwenda kujisaidia porini.
“ Vyoo ni vichache na
vichafu,ubaguzi na udhalilishaji kutoka kwa baadhi ya wahadhiri wenye asili ya
kihindi,tunapinga kuitwa majina ya mahudhurio darasani kila siku kama
inavyofanyika katika shule za msingi na sekondari sisi ni wanachuo wa chuo
kikuu,pia tunapinga kitendo cha chuo hiki kubadilisha masomo tuliopangiwa na Tume ya vyuo vikuu’’,alisema
mmoja wa wanachuo.
Walidai
kuwa chuo hicho kina vyoo vyenye matundu 14 kati ya matundu hayo saba ya
wanawake na saba ni wanaume ukilinganisha na idadi halisi ya wanachuo ambayo ni
zaidi ya 1,200 na kusababisha tundu moja
kutumiwa na wanachuo 64 badala ya 20 .
Walidai kuwa madai
hayo ndiyo yaliyosababisha uongozi wa
chuo kuwaondoa madarakani Rais na serikali yote ya chuo bila taarifa kwa
wanachuo ambao wameiweka madarakani hali
iliyosababisha mgomo na vurugu zilizosababisha chuo kufungwa kwa muda
usiofahamika.
Mkurugenzi na makamu St.Joseph wanena
Januari 20,mwaka huu
uongozi wa juu wa chuo kikuu cha mtakatifu Joseph ukiongozwa na Dk.Txa Ananth ambaye ni Rais wa
Baraza la vyuo vikuu vya mtakatifu Joseph Afrika vinavyomilikiwa na watawa wa
DMI ulitembelea chuo hicho na kubaini hakuna mawasiliano mazuri baina ya
uongozi wa chuo na wanachuo.
Kutokana na hali hiyo
viongozi hao wa juu wa St.Joseph walikubali kufungwa kwa chuo hicho ili kutoa
fursa ya kupatia ufumbuzi uliosababisha mgomo chuoni hapo na kuahidi kuundoa
uongozi wote wa chuo na kuboresha miundombinu yake.
Kwa upande wake
makamu mkuu wa chuo cha mtakatifu Joseph Sr.Antonia DMI amekiri kufungwa kwa
chuo hicho kwa muda usiojulikana kwa wanafunzi wanaosoma ngazi ya shahada huku
wanachuo wanasoma ngazi ya stashahada wakiendelea na masomo yao.
“Chuo kimefungwa
kutokana na vurugu na mgomo wa wanachuo ambao wamegoma kuingia drasani na
kufanya vurugu ikiwemo kuweka gundi aina
ya superglue kwenye kufuli za milango ya madarasa’’ ,alisema na kuongeza kuwa
mgomo huo pia umesababishwa na kuondolewa kwa serikali ya wanachuo akiwemo Rais
na katibu wake kwa kosa la kufanya mkutano bila taarifa kwa uongozi wa chuo.
Hata hivyo Sr.Antonia
amepinga madai ya wanachuo kubaguliwa,kudhalilishwa na kunyanyaswa na
kusisitiza kuwa kila kinachofanyika katika chuo hicho ni kwa mujibu wa sheria
za chuo ambazo pamoja na mambo mengine zinazuia mwanachuo kufika chuoni akiwa
na vifaa vya mawasiliano kama vile simu
na kompyuta.
Wanachuo
40 washikiliwa na polisi
WANANCHUO 40 wa chuo kikuu cha mtakatifu Joseph tawi la
Songea walishikiliwa na jeshi la polisi mkoani Ruvuma kwa kosa la kwa siku
mbili kwa kosa la kukusanyika katika eneo la chuo wakati chuo kimefungwa kwa
muda usiojulikana.
Chuo cha mtakatifu
Joseph tawi la Songea kilifungwa tangu
Januari 15,mwaka huu kutokana na vurugu na mgomo wa kuingia darasani wa
wanachuo wakidai madai mbalimbali.
Kamanda wa polisi
mkoani Ruvuma Deusdedith Nsimek alisema
siku ya Jumanne asubuhi majira ya saa mbili asubuhi wanachuo zaidi ya 300 walikusanyika katika chuo cha
mtakatifu Joseph kwa madhumuni ya
kufanya vurugu kwa madai kuwa hawatambui kama chuo kimefungwa wakitaka kuingia
chuoni.
Kamanda Nsimek
alisema wanachuo hao walipohojiwa na polisi kwanini wamekusanyika katika eneo
hilo,walianza kuporomosha matusi kwa askari na kuwarushia mawe ndipo
ikawalazimu askari kutumia nguvu ikiwemo kupiga mabomu ili kuwatawanya wanachuo
hao ambao idadi yao iliendelea kuongezeka.
Kamanda huyo wa
polisi mkoa wa Ruvuma alisema wanachuo walikataa kutii agizo la serikali badala
yake waliendelea kukusanyika eneo la
chuo kila siku licha ya ulinzi wa jeshi la polisi ulioimarishwa chuoni hapo
tangu kufungwa kwa chuo hicho.
Kulingana na Nsimek siku
ya tukio wanachuo walikusanyika na kuanza kurusha mawe kwa askari huku
wakiungwa mkono na makundi ya wanachuo waliokuwa wanatoka maeneo ya jirani
pamoja na waendesha pikipiki na kwamba licha ya kutangaziwa zaidi ya mara tatu
na polisi watawanyike kwa kuwa mkusanyiko wao haukuwa na kibali lakini
walikataa ndipo askari waliwatanya na kufanikiwa kuwakamata wanachuo 40.
“ Miongoni mwa
waliokamatwa ni Rais wa chuo hicho Aristides
Munjwahuzi,Rais wa chuo aliyeondolewa madarakani na uongozi wa chuo,
ameonekana kuwa ndiyo anawaongoza wenzake kukusanyika na kutotambua amri ya
kufungwa kwa chuo hicho’’,alisema.
Kauli
ya serikali ya mkoa kuhusu mgomo
Mnamo Januari 16 mwaka huu mkuu wa wilaya ya
Songea Joseph Mkirikiti akitoa tamko la
serikali kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu aliwaasa wanachuo
waache vurugu na kutawanyika ili kuheshimu maamuzi ya chuo kufungwa hadi hapo
madai yao yatakapopatiwa ufumbuzi kupitia Taasisi zinazohusika na elimu ya juu
Kufuatia mgogoro huo kuendelea serikali
ya mkoa wa Ruvuma imeingilia kati kwa kuita bodi ya chuo hicho na kukaa nayo na
imewataka wazimalize tofauti zao ili masomo yaweze kuendelea.
Akiongea na waandishi
wa habari ofisini kwake mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu
alisema kuwa serikali ya mkoa imeamua kuiita bodi ya chuo hicho na kuitaka
ikamalize tofauti hizo ambazo uongozi wa chuo hicho umekuwa ukilalamikiwa mara
kwa mara na wanachuo hao ambao wamedai kuwepo kwa kero nyingi ambazo
zimeshindwa kutekelezeka.
Mwambungu alisema kuwa chuo cha st.Joseph tawi la Songea kinahitaji kifanyiwe marekebisho makubwa ili kiende sanjari na vyuo vikuu vingine vya hapa nchini hivyo bodi ya wakurugenzi wa chuo hicho ni vyema iangalie uwezekano wa kukutana na Baraza la vyuo vikuu hapa nchini kwa lengo kuboresha mazingira ya chuo hicho ili kiendane na hadhi ya vyuo vikuu vingine.
Katika hatua nyingine
chuo hicho kimefikia hatua ya kulitia aibu kanisa katoliki nchini baada ya
baadhi ya wahadhiri kuanza kupigana wenyewe kwa wenyewe huku wakiumana meno
sehemu mbalimbali za mwili baada ya dean
wa wanachuo raia wa India aliyefahamika kwa jina moja la Nicholus kukataa
kusaini wanachuo 25 kufukuzwa chuo ambao wanadaiwa kuwa vinara wa mgomo.
Chuo kikuu cha
mtakatifu Joseph Songea kilianza mwaka 2004 kikiwa na wanachuo wachache ambapo
hivi sasa chuo hicho kina idadi kubwa ya wanachuo ambao ni 685 kati yao wanaume
ni 558 na wanawake 127 ambao wanasoma stashahada na shahada katika Sayansi ya
kompyuta.
Hata hivyo kuanzia
mwaka wa masomo uliopita chuo kimeanza kutoa
masomo ya shahada ya Sayansi ya elimu ambapo tayari kuna wanachuo 205
wanaosoma kozi hiyo na kwamba katika chuo hicho kampasi ya Songea tangu mwaka
2010 kinatoa masomo ya shahada ya
kilimo ambapo tayari kuna wanachuo 173
kati yao wanaume ni 119 na wanawake 54.
albano.midelo@gmail.com,simu
0784765917
No comments:
Post a Comment