Na Stephano Mango
Usafi wa Mazingira
unaofanyika kila siku katika manispaa ya
Songea kuanzia mwaka huu umeufanya mji huo kuwa kuvutia wengi na kuwa msafi kuliko kipindi kingine chochote cha uhai wa
manispaa hiyo.
Utafiti umebaini kuwa
manispaa ya Songea ambayo ndiyo kioo cha mkoa wa Ruvuma inaongoza kwa usafi
ukilinganisha na Halmashauri nyingine za mkoa huo ambazo ni Halmashauri za
Songea manispaa, Halmashauri ya wilaya ya Songea, Tunduru, Namtumbo, Madaba,
Nyasa,Halmashauri ya Mbinga na Mbinga
mji.
Ofisa habari wa
manispaa ya Songea Albano Midelo amesema tangu kutolewa kwa agizo la usafi wa
mazingira na sasa sheria ya usafi wa
mazingira katika nchi nzima kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kumeongeza moyo wa kujituma kwa wakaziwa
manispaa hiyo hivyo kuweka viunga vya mji
huo katika hali ya usafi wakati wote.Amesema licha ya manispaa ya Songea kukabiliwa na
changamoto ya uzalishaji taka nyingi kutokana na ongezeko kubwa la watu ambao ni zaidi
ya watu 203,309,,idara ya afya inafanya kazi ya ziada kuhakikisha mji huo unaendelea kuwa safi hasa kutokana na ukweli kuwa Songea ndiyo kioo cha mkoa wa Ruvuma.
ya watu 203,309,,idara ya afya inafanya kazi ya ziada kuhakikisha mji huo unaendelea kuwa safi hasa kutokana na ukweli kuwa Songea ndiyo kioo cha mkoa wa Ruvuma.
Midelo amesema
uongozi wa Halmashauri ya manispaa ya Songea umesikitishwa na upotoshaji
uliofanywa hivi karibuni na televisheni moja binafsi kupitia mwandishi wake wa
mkoa wa Ruvuma akidai kuwa uchafu umekithiri katika manispaa ya Songea jambo
ambalo sio taarifa sahihi.
“Kila mmoja ni
shahidi ukitembelea katika maeneo mbalimbali ya mji wa Songea,mazingira yake ni
ya kuvutia,usafi unafanyika kila siku,magari ya takataka yanasomba,ukisema mji
wa Songea ni mchafu ni udanganyifu wa hali ya juu’’,alisisitiza Midelo.
Ametoa wito kwa
wanahabari nchini kufanya kazi zao kwa mujibu wa maadili,kanuni na sheria za
uandishi wa habari kwa kuwa ni kosa kubwa kwa mwandishi kuandika habari ambazo
za upotoshaji kwa kuwa wanaweza kuchukuliwa hatua za kisheria.
Akizungumzia hatua ambazo zinaendelea kuchukuliwa na Manispaa
ya Songea katika kuhakikisha mazingira yanaendelea kuwa safi,Midelo anasema
Halmashauri imeamua kutumia makampuni kwa ajili ya kusimamia shughuli za usafi
wa mazingira ili kuhakikisha kuwa mji wa Songea unaendelea kuwa safi wakati
wote.
Amesema tayari Baraza la madiwani la manispaa hiyo kwa
pamoja wameunga mkono na kuidhinisha shughuli za usafi wa mazingira ndani ya
Halmashauri ya Manispaa ya Songea zifanywe kwa kutumia makampuni ili kuongeza
kasi ya usafi wa mazingira.
Hata hivyo amesema Baraza hilo limekubali viwango vya
adhabu itakayotokana na wachafuzi wa mazingira
iwe kwa mujibu wa Sheria ndogo ya usafi wa mazingira ya Halmashauri ya
Manispaa ya Songea ya mwaka 2015.
Kulingana na tangazo
la serikali Namba 308 la mwaka 2015, viwango vya utozaji faini kwa kila mkosaji
vitafuata Sheria ndogo ya mwaka 2015 ambayo inatamka mkosaji kulipa faini ya
papo kwa papo isiyopungua Shilingi 50,000 na akifikishwa mahakamani atalipa
faini isiyopungua Shilingi 100,000.
Mbunge wa jimbo la
Songea mjini Leonidas Gama ambaye amewahi kuwa mkuu wa mkoa wa
Kilimanjaro alieleza kuwa Manispaa ya Moshi imefanikiwa kwenye zoezi la usafi
baada ya kutumia Kampuni ambayo ndiyo inawajibika kwa Halmashauri.
Baraza la madiwani la
manispaa ya Songea limeshauri uwekwe mkakati wa kuwadhibiti wachafuzi wa
mazingira kwa kutumia kikundi cha askari wa usafi wa mazingira ambao watatoza
faini za papo kwa papo mara wamkamatapo aliyechafua eneo lolote.
Baadhi ya wakazi wa
mji wa Songea akiwemo Anna Komba na Joseph Ngonyani wamefurahia hatua
iliyochukuliwa na Baraza la madiwani wa manispaa ya Songea ambapo wamesema imebadilisha mji wa Songea kuonekana msafi na
kuvutia wakati wote ukilinganisha na hali ya miaka ya nyuma.
Mwisho.

No comments:
Post a Comment