NA
KWIRINUS MAPUNDA,SONGEA
Halmashauri ya
manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imefikia asilimia 95 katika utengenezaji wa
madawati hadi kufikia Juni 8 mwaka huu.
![]() |
| Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa George Mbijima |
Ofisa habari wa
manispaa hiyo Albano Midelo amesema manispaa hiyo katika kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kumaliza kero ya
madawati inaendelea kutengeneza na kukamilisha madawati 5,130 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 333.45 ambayo
yanahitajika katika manispaa ya Songea.
Hata hivyo amesema hadi
kufikia wiki ya kwanza ya mwezi Juni Madawati yote yaliyokwisha tengenezwa ni 4830
kati ya madawati 5130 ambayo
sawa na asilimia 94.2 ya mahitaji ya madawati yote.
Amesema Juni 8 mwaka huu kiongozi wa
mbio za mwenge kitaifa George
Mbijima alikabidhi madawati 100 yenye thamani ya shilingi milioni 6.5 katika Shule
ya msingi Luhira mchanganyiko ambayo ni miongoni mwa shule 81 za Serikali na
binafsi zilizopo katika Manispaa ya Songea.
“Shule hiyo ni ya Mchanganyiko
ina Wanafunzi wa kawaida 2031 kati yao Wanaume 991,wanawake 1040. Shule ina
Wanafunzi wenye ulemavu wa macho wapatao
40 kati yao wanaume 18,wanawake 22 hivyo madawati hayo yamemaliza kero ya
madawati katika shule hiyo ilioanzishwa mwaka 1928 ambayo pia waziri mkuu
mstaafu hayati Rashid Kawawa alisoma’’,alisema.
Kaimu afisa elimu wa manispaa ya Songea Sunday Wahyungi amesema Mradi
wa madawati katika manispaa hiyo ulianza tangu mwezi wa Desemba mwaka 2015 ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa
Jamhuri wa Muungano wa Tanzania iliyowataka
Wakuu wa Mkoa,Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuhakikisha kuwa hakuna
wanafunzi wanaokaa chini hadi kufikia Juni 30 mwaka huu.
Wahyungi
amesisitiza kuwa kabla ya Juni 30 hakuna mwanafunzi ambaye atakaa chini katika
shule za msingi za manispaa hiyo kwa kuwa madawati yote yaliopangwa kukamilisha
mradi wa madawati yatakuwa yametengezwa hivyo uhaba wa madawati katika manispaa
ya Songea kubakia kuwa historia.
Kwa upande wake mkuu
wa wilaya ya Songea Benson Mpesya amesisitiza kuwa hadi kufikia Juni 30 mwaka
huu miradi yote ya madawati katika wilaya hiyo itakuwa imekamilika hivyo
kumaliza kabisa tatizo la baadhi ya wanafunzi katika shule kukaa chini kutokana
na upungufu wa madawati.
Akizungumza na
watumishi wa Halmashauri zote tatu zinazounda wilaya ya Songea ambazo ni Songea
manispaa,Halmashauri ya Songea pamoja na Halmashauri ya Madaba amewaagiza
watendaji katika ngazi zote kusimamia zoezi la utengenezaji wa madawati
yaliobakia kabla ya Juni 25 ambayo inatarajiwa kuwa siku maalum ya kutoa taarifa
ya kumaliza utengenezaji wa madawati katika wilaya ya Songea.
Mwisho


No comments:
Post a Comment