Majengo mengi yamekamilika
HALMASHAURI ya manispaa ya Songea
imepitisha ombi la kituo cha afya cha mji mwema kupandisha hadhi kuwa
hospitali ya Halmashauri ya manispaa hiyo.
Hata hivyo alisema ombi la kupandisha hadhi Kituo hicho cha afya lilikuwa
ni agizo la waziri wa afya,ustawi wa
jamii,jinsia,watoto na wazee Ummy
Mwalimu alipotembelea kituo hicho Januari 11
mwaka huu.
Alisema Waziri Mwalimu aliagiza Ombi
la kupandisha hadhi Kituo cha Afya Mjimwema kuwa Hospitali ya Wilaya liwasilishwe
Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia,
Watoto na Wazee ili kupata idhini ya
Wizara yenye dhamana.
Afisa habari huyo alisema kikao cha
Baraza la madiwani kikiongozwa na Mstahiki Meya Abdul Hassan Mshaweji kilipokea
w taarifa na kikao kiliidhinisha
upandishaji hadhi Kituo cha Afya Mjimwema kuwa Hospitali ya Halmashauri ya
manispaa.
Amelitaja lengo la kuwa Hospitali ya
Wilaya ni kuboresha huduma mbalimbali za afya ambazo hazipatikani kwenye Kituo
cha Afya na sababu za msingi kuomba kuwa Hospitali ya Wilaya ni kuiwezesha
Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuwa na Hospitali ya Wilaya ambayo itaweza
kuhudumia wananchi wa Manispaa na wale wanaotoka Kata na Wilaya za pembezoni
Kituo cha Afya Mjimwema kilianzishwa Aprili
8,2002 ambapo Kituo hicho kinahudumia wakazi wanaokadiriwa kufikia 31,091 kati
ya hao 1213 ni watoto chini ya mwaka mmoja, 5845 ni watoto chini ya miaka
mitano, 1275 ni wajawazito wanaotegemewa na 7586 ni wanawake walio na umri wa
kuzaa.
Alisema Kituo cha afya cha Mjimwema
kina majengo nane yakiwemo Jengo la
wagonjwa wa nje, Wodi ya Watoto na Wanawake, Wodi ya Wazazi na huduma za
kujifungua, jengo la kutolea huduma za afya ya uzazi na mtoto na wodi ya
Wanaume, jengo la Utawala, jengo la kuhifadhia maiti, nyumba mbili za watumishi
na jengo la upasuaji.
Kulingana na ofisa habari huyo,Kituo
cha Afya Mjimwema kina jumla ya watumishi 110 wa kada mbalimbali na kwamba Kituo
kinatoa huduma mbalimbali za afya.
Hata hivyo alizitaja huduma ambazo
hazitolewi katika kituo hicho cha afya kuwa ni pamoja na Huduma ya upasuaji licha ya kwamba jengo
limekamilika lakini vifaa bado havitoshelezi kuanza huduma hiyo,huduma nyingine
ambazo hazitolewi ni huduma za macho, huduma za kuongeza damu, huduma za pua,
masikio na koo na huduma ya mionzi yaani ultrasound.
Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina
vituo 30 vinavyotoa huduma za afya ambavyo ni Hospitali moja, Vituo vya Afya
vitatu vikiwepo viwili vya Serikali na kimoja cha Shirika la Dini na Zahanati
26 Kati ya hizo Zahanati 19 zinamilikiwa na Serikali, zahanati mbili zinamilikiwa
na Mashirika ya Dini, na zahanati nne
zinamilikiwa na watu binafsi ambapo Zahanati moja inamilikiwa na UMATI.
Mwisho
Udah punya Asuransi belum? Pasti belum, iya kan. Yuk baca artikel berikut Asuransi Kendaraan MSIG, Berkendara Tanpa Cemas kali aja setelah baca artikel berikut langsung kepincut beli asuransi. Asuransi itu penting loh.
ReplyDelete