Saturday, April 30, 2011

Maadhimisho ya siku ya usalama na afya duniani yafana mjini Songea

Picha inaonyesha Blass Band ya jeshi la magereza mkoa wa Ruvuma ikiongoza maandamano siku ya maadhimisho ya  siku ya usalama na afya mahali pa kazi duniani ambazo kitaifa zimefanyika mkoani Ruvuma ambapo mgeni rasmi alikuwa na waziri wa  kazi na ajira Gaudentia Kabaka picha na Albano Midelo.

Wafanyakazi wa kampuni ya Bia Tanzania TBL wakishiriki katika maandamano hayo ambayo yalianzia kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa wa Ruvuma hadi uwanja wa michezo wa Majimaji mjini Songea.

Waziri wa kazi na ajira Gaudentia Kabaka akikabidhi tuzo kwa mwakilishi wa kampuni ya Bia Tanzania TBL  Bi.Rose Kailembo,shirika hilo ni miongoni mwa mashirika tisa ambayo yalishinda tuzo na kuwa washindi wa maswala ya afya na usalama mahali pa kazi picha na Albano Midelo.

Picha inaonesha baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Bia Tanzania TBL kutoka makao makuu pamoja na wafanyakazi wa TBL tawi la Ruvuma wakishangilia baada ya kukabidhiwa tuzo na waziri wa kazi na ajira  Gaudentia Kabaka kwenye uwanja wa michezo wa Majimaji wa Songea.

1 comment:

  1. Natoa hongera kwa sherehe hii, nikizingatia umuhimu wa elimu ya afya na usalama.

    Naona tangazo la bia hapo juu. Suala la bia ni tata, kwani bia ni chanzo au kichochezi cha ajali nyingi, na uharibifu wa maisha, mali, na afya za wengi. Nimewahi kuandika kidogo kuhusu suala hilo. Soma hapa.

    ReplyDelete