Gari la wizara ya maliasili na utalii likiwa lipepambwa na ngozi mbalimbali za wanyama wakiwemo chui,simba,pundamilia pamoja na mafuvu ya wanyama pamoja na wanyama halisi ambao walikuwa wamewekwa kwenye cage siku ya maadhimisho ya sherehe ya wafanyakazi Mei Mosi ambazo kimkoa zilifanyika wilayani Mbinga na mgeni rasmi alikuwa ni mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dk.Christine Ishengoma.Banda la maliasili lilikuwa kivutio cha aina yake hali iliyosababisha watu wengi kumiminika kwenye bando hilo picha na maelezo na Albano Midelo
Baadhi ya watoto wa shule za msingi wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wakiwa katika Banda la maonyesho la wizara ya maliasili na utalii wakishangaa baadhi ya wanyama pamoja na kupata maelezo kuhusu wanyama hao kutoka kwa wataalamu wao walipotembelea kwenye banda hilo picha na maelezo na Albano Midelo.
Mkuu wa kikosi cha kuzuia ujangili kanda ya kusini Metson Mwakanyamale akiendelea kutoa maelezo kuhusu shughuli zinazofanywa na wizara ya maliasili na utalii kwa watu waliotembelea banda lao la maonyesho ambalo liliwavutia wengi waliotembelea picha na Albano Midelo.
No comments:
Post a Comment