Na
WIZARA ya afya na ustawi wa jamii imelitangaza jiji la mwanza kukamata nafasi ya kwanza katika shindano la afya na usafi wa mazingira katika Halmashauri za jiji hapa nchini katika kipindi cha mwaka 2011.
Picha inaonesha
mshindi wa jumla wa usafi kitaifa mkoa wa Iringa ambao licha ya kupewa tuzo na zwadi mbalimbali lakini pia walikabidhiwa kombe la ushindi
Mganga mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dk.Daniel Malecela akisoma hotuba ya waziri wa afya na ustawi wa jamii nchini Dk.Hadji Hussein Mponda siku ya kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira duniani ambazo zilifanyika kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea,alisema jiji la Mwanza limeibuka kidedea baada ya kuyashinda majiji ya Dar es salaam na Mbeya .
Waziri wa afya alilitaja kundi la pili ambalo limeshinda katika shindano la afya na usafi wa mazingira kuwa ni manispaa ya Moshi ambayo imekamata nafasi ya kwanza kati ya Halmashauri za manispaa 17 nchini ambapo manispaa ya Arusha imeshika nafasi ya pili na mshindi wa tatu ni manispaa ya Iringa.
Mshindi wa kwanza katika nafasi ya Halmashauri za miji nchini kati ya miji sita iliyoshiriki, imechukuliwa na mji wa Mpanda,nafasi ya pili ni mji wa Njombe ambapo katika Halmashauri 20 za wilaya zilizoshiriki katika shindano hilo ,Halmashauri ya wilaya ya Njombe imekamata nafasi ya kwanza na kufuatiwa na Halmashauri za Meru na Rungwe.
Washindi wote walizawadiwa zawadi zenye thamani tofauti kwa kuzingatia nafasi ya ushindi na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo waziri wa ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi profesa Anna Tibaijuka ambaye alimwakilisha waziri mkuu Mizengo Pinda.
No comments:
Post a Comment