Na Mwandishi maalum
WAANDISHI wa habari wawili kutoka mkoani Ruvuma wameibuka miongoni mwa washindi sita katika mchuano mkali wa kupata tuzo ya Fellowship inayotolewa na mfuko wa ruzuku kwa vyombo vya habari Tanzania (TMF).
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam meneja wa TMF Erenest Sungura aliwataja washindi hao sita kuwa ni pamoja na Albano Midelo mwandishi wa kujitegemea kutoka Ruvuma Editha Karlo mwandishi wa New Habari kutoka mkoa wa Ruvuma,Damasi Kanyabwoya wa The Citzen,Latifa Ganzel wa Uhuru na Mzalendo,Mariam Omary wa Zanzibar Leo na Daniel Mbega wa Mwanasipoti.
Kwa mujibu wa Sungura ushindani wa tuzo hiyo ya Fellwship ulikuwa mkubwa ambapo awali walijitoeza waandishi wengi kutoka katika mikoa mbalimbali nchini ambapo waliofanikiwa kuingi akatika raundi ya pili walikuwa ni waandishi 26 na kwamba washidi hao wamepatikana baada ya jopo la majaji ambao ni wahariri wa vyombo mbalimbali kuwafanyia usaili wa aina kwa ana na kuandika.
Sungura alibanisha zaidi kuwa washindi hao sita chini ya mpango wa Fellowship watafanyakazi chini ya wakufunzi waliobobea katika fani za habari kwenye sekta ya kilimo na mazingira ambapo wakufunzi hao watatoka ndani na nje ya nchi.
“Washindi hawa sita wa fellowship watapewa ruzuku ya shilingi milioni mbili kwa mwezi ambazo zitawasaidia katika tafiti zao pamoja na gharama za kuishi katika kipindi chote cha programmu hiyo ambayo itadumu kwa miezi sita,pia watapewa vitendea kazi muhimu vikiwemo kamera ya kisasa,kompyuta(laptop) pamoja na vinasa sauti”,alisisitiza.
Mpango wa fellowship hufanyika mara moja kwa mwaka ambapo waandishi wanaokuwa wameshinda katika mpango huo wanajengewa uwezo zaidi na hasa katika eneo maalum ili kuongeza ubora wa uandishi wa habari za uchunguzi na zile zenye maslahi kwa umma.
Kwa maoni niandikie awamufill@gmail.com
No comments:
Post a Comment