Thursday, March 8, 2012

Mfahamu Daktari anayetibu magonjwa kwa matunda

i  
 Na Albano Midelo
Christopher Michael ni daktari wa  mimea,binadamu na wanyama ambaye amesomea nchini Marekani kwa miaka nane, anafanya utafiti wake wa miaka mitatu mkoani Ruvuma anasema matumizi ya kemikali  kama bluekopper kupulizia jirani na vyanzo vya maji  vinasababisha magonjwa zaidi ya 30 kwa binadamu na kwamba tiba ya magonjwa hayo ni gharama kubwa.

Anabainisha kuwa magonjwa yanayosababishwa na kula au kunywa kemikali au sumu aina ya bluecopper hayatibiki kwa urahisi ndiyo maana wagonjwa wengi wanaoathirika na sumu wanaweza kupata matibabu nje ya nchi hususani nchini India kwa gharama kubwa.


Hata hivyo amesema mtu ambaye ameathirika na bluecopper anaweza kutambuliwa kwa kati ya miezi mitatu hadi miaka miwili kutegemea na aina ya ugonjwa aliougua ambapo ameyataja baadhi ya magonjwa ambayo mtu anaweza kuugua kwa kunywa au kula kemikali hiyo kuwa ni ugonjwa wa ini,saratani ya damu, figo, ngozi,kuoza sehemu za siri, kupata mzio, kuoza mapafu,  macho, magonjwa ya kuhara, amiba, kichocho, kuvimba tumbo, ugonjwa wa moyo ambao humpata mwanamke wakati wa kujifungua.

Kwa mujibu wa Dk.Michael dalili za mtu ambaye ameathirika na  madhara yanayoletwa na matumizi ya bluekopper ni magonjwa ya ngozi,kung’oka kwa kucha,kuumwa ugonjwa wa macho aina ya trachoma,kope kuwasha, kupoteza uwezo wa kuona kushindwa kusoma na kuandika,chembechembe hai za damu kuungua,kuoza mapafu,kiharusi,kuharibika figo, kukosa hewa kwenye ubongo,kupoteza fahamu na matatizo ya akiri.
  
“Bluecopper ikiingia mwilini hakuna dawa za kuweza kuiondoa sumu hiyo ,kinachofanyika hospitalini ni mtu ambaye anakuwa na dalili kwa mfano za kupoteza fahamu anapewa dripu la maji ,tatizo la kuathirika na blue copper lipo kila mahali kwenye vyanzo vya maji  vilivyochafuliwa kutokana na shughuli za kibinadamu, kinachotakiwa ni kutoa elimu ya kutochafua maji kwenye vyanzo ’’,anasisitiza.
albano.midelo@gmail.com,simu 0766463129


No comments:

Post a Comment