Na Albano
Midelo
Akihubiri kwa nyakati
tofauti siku ya mkesha wa sikukuu ya Pasaka na Jumapili ya pasaka kwenye kanisa
la kiaskofu la mtakatifu Mathias Kalemba mjini hapa alisisitiza kuwa kiongozi
ambaye sio mkweli hawezi kuongoza
taasisi ya aina yeyote ile iwe ya kidini au kijamii.
Kwa mujibu wa
mhashamu Mtega mafundisho na maagizo ya
Yesu kristo daima yalizingatia ukweli na kwamba mafundisho hayo yanatakiwa
kutumika kwa binadamu wote ulimwenguni wakiwemo wale ambao wamepewa dhamana ya
kutawala.
Hata hivyo alisema dola nyingi zinawakandamiza watu wanyonge huku viongozi
wachache wakiendelea kujipatia utajiri ambao hauwajali kwa kushindwa kuwatimizia mahitaji ya muhimu katika maisha ya binadamu.
“Utawala wa namna hii
una mambo ya kisanii,kwa kuwa daima hauzingatii ukweli na maamuzi yake
yanakuwa hayana ukweli jambo ambalo ni
kinyime na maagizo ya kristo mwenyewe’’,alisema.
Mhashamu Mtega
alibainisha kuwa leo waumini wa kanisa katoliki ulimwenguni wanapoadhimisha
ufufuko wa Yesu kristo wawe mstari wa mbele kwa kutoa ushuhuda na kuheshimu sakramenti na kudumu katika
maisha ya sara,kuhudhuria jumuiya ndogo ndogo na kujenga tabia ya kusoma Biblia
takatifu.
Katika hatua nyingine
mshamu Mtega alikemea tabia ya baadhi ya
watu wanaopotosha ukweli kuhusu kufa na kufufuka kwa Yesu kristo na kusisitiza
kuwa anayemkashifu ufufuko wa Yesu ni
shetani kwa kuwa Yesu ni Mungu kweli na
alifufuka kweli.
“Kuna nabii gani amewahi kufa na kufufuka zaidi ya mwokozi
wetu Yesu Kristu?alihoji Askofu mkuu Mtega. Katika nafasi hiyo alikemea pia
tabia iliyozoeleka ya watu waliopewa dhamana kuomba rushwa na kusisitiza
kuwa tabia hiyo inawanyima haki watanzania wengi wanyonge .
albano.midelo@gmail.com
No comments:
Post a Comment