Na Albano
Midelo,
WATU 130 wakiwemo wa
madhehebu mbalimbali wamejiandikisha kwenye kamati ya mchakato wa Sista Bernadeta Mbawala kwa ajili ya kutoa
ushuhuda wao namna walivyotendewa na
mtumishi huyo wa Mungu katika maisha yao.
Akihubiri katika kanisa
kuu la kiaskofu la mtakatifu Mathias Kalemba la mjini hapa Jumapili wiki hii
paroko wa parokia ya Songea padre Ananias Mbawala alisema kamati ya mchakato
bado inaendelea kupokea majina ya watu ambao watatoa ushuhuda katika maisha yao
uliotokana na maombezi ya mtumishi wa
Mungu Sr.Bernadeta.
Kwa mujibu wa paroko
hao wata watatoa ushuhuda wao katika mambo mbalimbali baada ya kusali na
kufanya maombezi kutumia kupitia mtumishi wa Mungu Sr.Bernadeta Mbawala na
kufanikiwa katika maisha.
“Baadhi ya matatizo
ambayo wamefanikiwa ni pamoja na wale ambao walishindwa kupata watoto kwenye
ndoa zao kwa muda mrefu wamefanikiwa kuwa na watoto,wengine wamefanikiwa kwenye
masomo yao,kupata ajira na wazazi wengine watoto wao ambao walikuwa na tabia
mbovu sasa wamekuwa watoto wenye maadili na kuwa mfano bora katika jamii na
wengine wamepona magonjwa sugu yaliokuwa yanawasumbua kwa miaka
mingi’’alisisitiza.
Paroko huyo
alibainisha zaidi kuwa katika kipindi hiki cha
sikukuu ya pasaka ambayo waamini wa kanisa katoliki wanaadhimisha
ufufuko wa Yesu Kristo ni vema waumini
wakasherehekea sikukuu hii kwa kuonyesha ushuhuda katika maisha yao na
kusisitiza kuwa injili inaendana na
ushuhuda.
Katika hatua injini
wakati mchakato wa kumtangaza Sr.Bernadeta kuwa mwenyeheri na hatimaye
mtakatifu kuanzia wiki ijayo ujenzi utaanza wa eneo la kuweka masalia ya
mtumishi huyo wa Mungu ndani ya kanisa
kuu la kiaskofu la Songea.
Paroko wa parokia ya
Songea padre Mbawala alisema eneo ya ujenzi
wa kuweka masalia hayo tayari limeandaliwa na kwamba hivi sasa waumini
wanahamasishwa kuchangia ujenzi huo ili uweze kukamilika kwa wakati.
Uzinduzi wa mchakato
wa kumtangaza Sista Bernadeta Mbawala
kuwa Mwenyeheri ulizinduliwa rasmi na
Askofu mkuu wa jimbo kuu katoliki la Songea mhashamu Norbert Mtega katika
kanisa kuu la kiaskofu la mjini Songea mapema mwaka huu.
Makao
makuu ya kanisa katoliki Vatican hivi
karibuni yametoa ruhusa kwa jimbo kuu katoliki la Songea kuanza mchakato wa
utafiti kuhusu maisha,fadhila za
uhodari,sifa ya utakatifu na nguvu za kimaombezi za Sista Bernadeta Mbawala ili
aweze kutangazwa kuwa mwenyeheri na hatimaye mtakatifu.
Sista Bernadeta
aliyezaliwa Oktoba 27,1911 katika kijiji cha Likuyufusi wilayani Songea
mkoani Ruvuma alifariki Novemba 29,1950
na kuzikwa katika makaburi ya Abasia ya
Peramiho yaliopo kilometa 24 kutoka mjini Songea
albano.midelo@gmail.com

No comments:
Post a Comment