Thursday, April 5, 2012

Mwambungu atoa vifaa kwa Mlale JKT


Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu
Na Albano Midelo 
OFISI ya mkuu wa mkoa wa Ruvuma imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya michezo vyenye thamani ya sh.milioni 2.5 kwa ajili ya kuisaidia timu ya soka ya JKT Mlale iliyofuzu tisa bora ligi kuu Taifa daraja la kwanza.
Akitoa msaada huo mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu alibainisha vifaa hivyo kuwa ni pamoja na  viatu pea 25 vyenye thamani ya shilingi milioni 1.5 na mipira 16 yenye thamani y ash.zaidi ya milioni moja.
“Ofisi yangu imeamua kutoa vifaa kwa lengo la kuitia moyo na kuiombea timu ya JKT Mlale iweze kufanya vizuri katika hatua ya tisa bora ili hatimaye iweze kucheza ligi kuu Tanzania bara msimu ujao’’,alisisitiza.
Akipokea msaada huo kwa niaba ya mkuu wa kikosi cha jeshi la kujenga Taifa Mlale sajenti Isack Msaigwa aliishukuru ofisi ya mkuu wa mkoa wa Ruvuma kwa msaada huo ambao alisema utasaidia kwenye maandalizi ya kushiriki ligi daraja la kwanza Tanzania bara hatua ya tisa bora.
Naye mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Ruvuma Joseph Mapunda alisema kuwa timu ya JKT Mlale ndiyo timu pekee ambayo inayoweza kuutangaza vema mkoa wa Ruvuma katika soka baada ya kushuka daraja timu ya Majimaji.
albano.midelo@gmail.com,simu 0766463129

  

No comments:

Post a Comment