Wednesday, October 3, 2012

Saratani tishio kwa nchi za Afrika


                         
UGONJWA wa saratani umekuwa tishio katika nchi za Afrika zilizo chini ya Jangwa la Sahara ikiwamo Tanzania ambapo kwa mwaka 2010, takwimu zinaonesha umeua watu milioni 9.9 duniani.
Hayo yalibainishwa na mratibu wa kampeni ya kupambana na ugonjwa huo nchini kutoka Taasisi ya Tanzania 50 Plus, Mchungaji Dk. Emmanuel Kandusi, alipozungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam.
Alisema saratani ni hatari sana ukilinganisha na takwimu za magonjwa mengine ambapo malaria uliua watu 500,000, kifua kikuu milioni 2.1, ukimwi milioni 1.8. Saratani inaongoza kwa kuua watu milioni 9.9.
Alisema asilimia 75 ya watu waliokufa kwa ugonjwa wa saratani (sawa na milioni 7.4), walitoka katika nchi zinazoendelea.
Akizungumzia dalili za saratani ya tezi dume, alisema mgonjwa hupata udhaifu katika kujisaidia haja ndogo, hisia ya kutaka kupata haja ndogo kila wakati hasa nyakati za usiku, mkojo kutoka wenyewe, maumivu au kuhisi muwasho wakati wa haja ndogo na uume kusimama kwa shida.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa jarida la Man, alisema ugonjwa huo unachangiwa na vyakula vyenye mafuta vikiwemo, nyama, chips mayai, pombe na kutofanya mazoezi ya viungo.
CHANZO TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment