WATOTO wote pacha watano waliozaliwa mwishoni mwa wiki katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma wamefariki usiku wa kuamkia jana .
Watoto hao wote
watano walizaliwa salama na Sophia Mgaya (28) mkazi wa Ruhuwiko mjini hapa kwa kufanyiwa upasuaji katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma.
Mganga mkuu Mfawidhi
wa Hospitali ya mkoa Songea(HOMSO)Dkt. Benedict Ngaiza, alisema kuwa watoto hao
wameishi kwa masaa kumi tu na kufariki dunia kutokana na kuzaliwa na uzito mdogo wa chini ya kilo moja.
Dkt.Ngaiza alibainisha kuwa watoto wote wanaozaliwa
wakiwa na uzito mdogo wanakuwa na maisha mafupi,hata hivyo alisema hali ya mama
wa watoto hao inaendelea vizuri ingawa bado amelezwa katika hospitali ya mkoa
wa Ruvuma akiendelea kupata matibabu..
Tukio ambalo
halijawahi kutokea katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma limetokea Mei 24 mwaka huu majira ya saa 4
asubuhi huku mtoto wa kwanza akiwa na
uzito wa gramu 730,wa pili 810,watatu 670,wanne 820 na watano gramu 430.
Kulingana na mganga
huyo kati ya watoto hao waliozaliwa,watatu ni wa kiume na wawili ni wa
kike na kwamba huu ulikuwa ni mzao wa
pili kwa mwanamke huyo.
Alieleza kuwa katika
mzao wa kwanza wa mama huyo alifanikiwa kujifungua mtoto mmoja na katika mzao
wa pili amebahatika kujifungua watoto
hao watano ambao wote wamefariki dunia .
Wakati huo huo jeshi la Polisi mkoani Ruvuma kwa kushirikiana na
Askari Wanyama Pori linamshikilia mtu mmoja kwa tuhuma za kukamatwa na
pembe za ndovu 11 zenye thamani ya shilingi milioni 38.8.
Kamanda wa polisi wa
mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsemeki,alisema tukio hilo lilitokea hivi karibuni huko katika kijiji cha Mandepwende Wilayani
Namtumbo.
Nsemeki alimtaja mtu
aliyekamatwa kuwa ni Issa Omar Mayono(57)mkazi wa Namtumbo na kudai kwamba
alipatwa na mkasa huo baada ya Askari mwenye namba 8057 D/SSGT Amily,akiwa
doria na askari wanyama pori ambao ni Joseph Luben(43) Daud Tesha(30) na Joseph
Abdalah(57) wote wakazi wa Msamala mjini Songea.
Alisema mtuhumiwa
huyo alikamatwa na Nyara hizo za Serikali zilizokuwa na uzito wa kilogram 42.6
wakati akiwa anasafirisha kutoka porini katika kijiji cha Mandepwende
kuelekea mjini Namtumbo.
Matukio ya kukamatwa kwa nyara za Serikali katika mkoa wa Ruvuma yamekithiri kutokana na watu wengi wasiokuwa na maadili na kufuata sheria kuuwa wanyama bila ya kuwa na vibali jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Matukio ya kukamatwa kwa nyara za Serikali katika mkoa wa Ruvuma yamekithiri kutokana na watu wengi wasiokuwa na maadili na kufuata sheria kuuwa wanyama bila ya kuwa na vibali jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Mwezi mmoja uliopita kampuni
ya Game Frontiers Tanzania(GFT) inayojishughulisha na uwindaji wilayani
Namtumbo kwa kushirikiana na kikosi cha askari wanyamapori katika pori la akiba
la Selous, walifanikiwa kukamata pembe za ndovu 15 zenye thamani ya shilingi milioni 192.
Kamanda huyo wa
polisi alisema mtuhumiwa anatarajia kufikishwa Mahakamani mara baada ya
upelelezi wa shitaka hilo kukamilika ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye
tabia kama hizo.
albano.midelo@gmail.com
albano.midelo@gmail.com

No comments:
Post a Comment