Na Fransis Godwin,Iringa
![]() |
| Kushoto ni Albano Midelo akikabidhiwa tuzo mbalimbali |
WAZIRI
wa maliasili na utalii Balozi Khamis Kagasheki amekabidhi kwa mara ya kwanza
tuzo za umahili wa uandishi bora wa habari za uhifadhi zilizoandaliwa na
shirika la hifadhi ya Taifa (TANAPA
2012 TANAPA MEDIS AWARDS
Aliwataja
walioshinda upande wa magazeti kundi la uhifadhi mshindi wa kwanza ni Albano
Midelo mwandishi wa kujitegemea wa Nipashe /Kiongozi aliyezawadiwa cheti ,hundi
ya Tsh milioni 1.5 ,ngao na safari ya siku saba katika nchi za kusini mwa
Afrika kwa kujifunza masuala ya hifadhi, Mussa Juma (Mwananchi) aliyeibuka
mshindi wa pili alipata cheti,hundi ya Tsh milioni 1 na watatu ni David Azaria –Habari
Leo alizawadiwa cheti na hundi ya Tsh.500,000.
Mshindi
wa kwanza upande wa Radio ni Alex Magwiza -TBC aliyezawadiwa cheti ,ngao ,hundi
ya Tsh milioni 1.5 na safari ya siku saba katika nchi za kusini mwa Afrika .

Wakati
katika luninga upande wa uhifadhi mshindi wa kwanza alikuwa mshindi mmoja pekee
Festo Sikaganamo (ITV) aliyeshinda ngao,hundi ya Tsh milioni 1.5 na safari ya
kujifunza utalii nchi za kusini mwa Afrika.
Wakati
tuzo ya utalii wa ndani upande wa magazeti mshindi wa tatu ni Elia Mbonea
(RAI)cheti na hundi ya Tsh 500,000,mshindi wa pili ni Salome Kitomari (Nipashe)
aliyepata cheti na hundi ya Tsh milioni 1 na mshindi wa kwanza alikuwa Phinias
Bashaya -Mwananchi aliyeshinda ngao,hundi ya Tsh milioni 1.5 na safari ya
kujifunza utalii nchi za SADC.
Eneo
la utalii wa ndani vipindi vya radio wa kwanza ni Alex Magweza (TBC)
aliyeshinda ngao,hundi ya Tsh milioni 1.5 na safari ya kujifunza utalii nchi za
kusini mwa Afrika na wa pili David Rwenyagira (Radio One) aliyepata cheti na
hundi ya Tsh milioni moja.
Upande wa utalii wa ndani katika TV mshindi wa tatu ni Juma Nugaz ( Clouds Tv) cheti na hundi ya Tsh 500,000, ,mshindi wa pili ni Raymond Nyamwihula (Star TV) wakati mshindi wa kwanza ni Lilian Shirima (TBC)
Akizungumza
baada ya kukabidhi tuzo hizo katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Wiloles
HIlltop mjini Iringa waziri Kagasheki alisema kuwa lengo la TANAPA kuanzisha tuzo
hizo kwa wanahabari ni kutaka kuona wanahabari wanaandika kwa usahihi na ubora
mkubwa habari za uhifadhi ikiwa ni pamoja na kufichua vitendo vya ujangili
katika hifadhi hizo .
Waziri
Kagasheki amewaasa wanahabari ambao wameshinda tuzo hizo na wale ambao
hawakushinda kuendelea kuandika habari za uhifadhi na pale wanapatakiwa
kushiriki katika shindano kujitokeza kushindanisha kazi zao.
"Shabaha
ya wizara kuanzisha tuzo hizi ni kuwapa moyo wanahabari nchini kote wa
kuendelea kuifanya kazi hiyo kwa ubora ikiwa ni pamoja na kufanya tafiti mbali
mbali"
Hata
hivyo amewashauri TANAPA kuendelea kuboresha zaidi tuzo hiyo kama njia ya
kuwawezesha wanahabari wengi zaidi kujitokeza ili mwisho wa siku kuweza
kuieleza dunia juu ya uhifadhi unaofanywa na Taifa katika uhifadhi kwa kuwa
wizara yake inawategemea zaidi wanahabari na vyombo vya habari katika kupambana
na vitendo vya ujangili.
Katika hatua nyingine waziri Kagasheki
aliutaja mkakati wa wizara yake ni kuitisha mkutano mkubwa wa wadau wa utalii
utakaofanyika mwezi Novemba mwaka huu kwa ajili ya kutafuta njia sahihi ya
kudumu katika kutokomeza ujangili wa wanyama katika hifadhi hapa nchini .
Alisema
kuwa tatizo la kuuwawa kwa Tembo duniani ni kubwa katika nchi ya Botswana na
Tanzania ni ya pili hivyo haitapendeza mikutano mikubwa ya kupambana na
ujangili kufanyika nchi za ulaya ambazo hakuna tatizo hilo badala ya nchi
husika kama Tanzania.
Pia
alisema kuwa mbali ya wizara yake kuanzisha utaratibu huo wa kuwapongeza
wanahabari wanaosaidia katika kuhamasisha uhifadhi na kufichua vitendo vya
ujangili bado anapongeza jitihada kubwa zinazofanywa na vyombo vya habari
nchini katika kukemea vitendo vya ujangili nchini .
Awali
meneja Uhusiano wa TANAPA
Paschal Shelutete alisema kuwa awali
tuzo hizo zilikuwa zikitolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) ila kutokana
na tathimini waliyoifanya wao wakaona ni vema tuzo hizo kuzitoa katika orodha
ya tuzo za MCT na kuzifanya wenyewe TANAPA .
Alisisitiza kuwa lengo la TANAPA ni kuona habari
zinazoandikwa zinakuwa na ubora wa hali ya juu na zinaendana na malengo ya
Taifa katika uhifadhi hivyo katika mwaka huu ambao ni mwaka wa pili kuzitoa
zoezi la kuwapata washindi wa tuzo hizo lilisimamiwa na jaji mkuu Dr.Ayub Rioba
pamoja na majaji wengine ambao wamebobea katika tasnia ya habari na masuala ya
hifadhi.
Tuzo hizo zilihudhuria na wahariri wa habari kutoka
vyombo karibu vyote nchini vya magazeti,radio na televisheni.
.CHANZO BLOG YA FRANSII GODWIN.

No comments:
Post a Comment