![]() |
| Dk.Reginald Mengi |
- Vinara wa rushwa nchini wadaiwa kulindwa
- Vigogo wannewatajwa kuhusika na mtandao
- MWENYEKITI Mtendaji wa Makampuni ya IPP, B w. Reginald Mengi, am esema ipo hatari ya Tanzania kuongozwa na viongozi watoa rushwa amba o baadhi yao wapo mahakamani lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi yao.Bw. Mengi aliyasema hayo DaresSalaam katika mkut ano wa majadiliano ul ioshirikisha wadau wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TP SF) na Ser ikali.
Alisema
kuna watu wanne ambao ni wakubwa(hakuwataja majina), ambao wan ashindwa
kudhibiti vitendo vya rushwa kwa sababu wao ni wahusika wakubwa katika mtandao
huo.
“Hapa
Tanzania kuna kitu kinaitwa utashi wa siasa wahusika wanamaanisha kupi ga vita
rushwa... jambo hili linafanyika kwa maneno si vitendo kwani asilimia kubwa ya
watu wa ngazi za juu ndio wahusika wakubwa wajanga hili.
“Kwa mawazo yangu na maeneo niliyopita, kuna wakubwa wanne hapa
nch ini ambao ndio vinara wa mtandao wa rushwa lakini hakuna mtu yeyote
anayewataja kutokana na nafasi zao,”alisema Bw.Mengi.
Aliong eza kuwa,asilmia kubwa ya watoaji rushwa ni watu wanaofanya
biashara ya dawa za kulevya nchini na kuwapa vijana ili waziuze hivyo kuhari bu
maisha yao na wengine hujikuta wakikamatwa katika nchi mbalimbali.
“Tatizo la rushwa pia lipo kwa viongozi wajuu ambao ndio wahusika
wakubwa wa mtandao huu... ni vyema vita ya rushwa na dawa za kulevya ikafanywa
kwa vit endo ili kuharakisha maendeleo ya nchi, ”alisema
CHANZO GAZETI LA MAJIRA

No comments:
Post a Comment