Na Albano Midelo
Umati mkubwa wa watu ulikusanyika
mjini Vatican kushuhudia tukio la kihistoria ambapo viongozi wawili wa zamani
wa Kanisa Katoliki, Papa John Paul II na Papa John XXIII wametangazwa
watakatifu.
Ibada ya misa takatifu
iliyoendeshwa kwa pamoja kati ya Papa Francis na mtangulizi wake Papa Benedict
XVI imeangaliwa na karibu mahujaji milioni moja
na wengine mamilioni ya watu kupitia matangazo ya vyombo mbalimbali vya habari duniani kote.
Karibu ujumbe wa wageni 100 wamehudhuria sherehe hiyo, wakiwemo kutoka koo za kifalme na wakuu wa nchi na serikali.
na wengine mamilioni ya watu kupitia matangazo ya vyombo mbalimbali vya habari duniani kote.
Karibu ujumbe wa wageni 100 wamehudhuria sherehe hiyo, wakiwemo kutoka koo za kifalme na wakuu wa nchi na serikali.
Kumbukumbu za kanisa katoliki zinaonyesha kuwa hii ni mara ya kwanza kwa papa wawili kutangazwa kwa wakati mmoja kuwa watakatifu.
Kanisa katoliki duniani limesema bado linaendelea na mchakato wa kuwatangaza kuwa watakatifu hayati mwalimu Julius Nyerere na Sr.Benadeta Mbawala wa Songea na kwamba mchakato ngazi ya Vatican unaendelea vizuri kwa kuzingatia hatua zote muhimu za mchakato.
CHANZO MSAADA WA MTANDAO

No comments:
Post a Comment