Na Julius Konala,Songea
Maandalizi ya mbio za
Mwenge wa Uhuru mwaka 2016 katika manispaa ya Songea mkoani Ruvuma yamepamba
moto kwa kuhakikisha miradi yote
inayotarajiwa kuwekewa mawe ya msingi na kuzinduliwa inakamilika.
![]() |
| Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Benson Mpesya akikagua stendi |
Ofisa habari wa
manispaa ya Songea Albano Midelo alisema Mwenge wa Uhuru katika manispaa hiyo
unatarajiwa kuingia Juni 8,2016 ukitokea wilayani Namtumbo ambao utakimbizwa
katika maeneo mbalimbali yenye miradi na
utakesha katika mtaa wa Kibulang’oma kata ya Lizaboni.
Kwa mujibu wa ratiba
ya Mwenge wa Uhuru katika manispaa ya Songea,Juni 9,2016 yatafanyika
makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru kati ya Halmashauri ya manispaa ya Songea na
Halmashauri ya mji wa Mbinga.
Kamati ya ulinzi na
usalama ya wilaya ya Songea ikiongozwa na mwenyekiti wake mkuu wa wilaya hiyo
Benson Mpesya pamoja na mkurugenzi wa manispaa ya Songea Jenifer Omolo
inaendelea kukagua miradi yote ambayo inatarajiwa kuwekewa mawe ya msingi na
kuzinduliwa katika manispaa hiyo.
Miongoni mwa miradi
hiyo ni pamoja na mradi wa madawati katika shule ya msingi Luhira,kuweka jiwe
la msingi mradi wa barabara ya lami ya FFU hadi Chemchem na uzinduzi wa nyumba
ya mkurugenzi wa manispaa ya Songea.
Miradi mingine ni
uzinduzi wa kituo cha mabasi cha mjini kati,uzinduzi wa darasa la matokeo makubwa sasa(BRN) katika shule
ya sekondari ya Chaburuma,mradi wa hifadhi ya mazingira Luhira na kukagua mradi
wa kikundi cha ufugaji kata ya Mwengemshindo.
Akizungumza wakati wa
ukaguzi wa miradi ambayo inatarajiwa kuwekewa jiwe la msingi na kufanyiwa
uzinduzi wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru katika manispaa ya Songea,mkuu wa
wilaya ya Songea Benson Mpesya amewaasa wakazi wa manispaa ya Songea kujitokeza
kwa wingi siku hiyo hasa kutokana na umuhimu wa Mwenge wa Uhuru.
“Mwenge wa Uhuru wa
sasa umelenga kuleta hamasa ya kuleta mabadiliko kwa kuhamasisha miradi
mbalimbali ya maendeleo ili wakazi wa Songea na watanzania kwa ujumla waweze kupata maendeleo
ya kweli hivyo ni vema wakazi wa Songea kujitokeza kwa wingi katika tukio hilo
ambalo linatokea mara moja tu kwa mwaka’’,alisisitiza.
Mwisho


No comments:
Post a Comment