Monday, May 23, 2016

Wanasayansi watumia nguruwe kutibu upofu



Wanasayansi wa Uchina wamefaulu katika tiba yao mpya ya majaribio ya kutibu upofu.

Walitumia nguruwe katika majaribio hayo ya tiba ya kuondoa upofu, ambapo walitumia konea kutoka kwa wanyama hao.
Sasa wamesema wana imani kwamba hilo litafaa sana kutokana na uhaba wa konea za binadamu.

Inakisiwa kuwa Wachina wapatao 5 milioni wanakabiliwa na matatizo ya konea, sehemu ya mbele ya jicho iliyo ngumu na inayowezesha miali ya mwanga kupenya.
Matatizo ya konea husababisha watu wengi kuwa kipofu.
 CHANZO BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment