Saturday, May 14, 2016

Ukame wasababisha Zimbabwe kuuza wanyamapori



Wanyama wengi wanakufa na kuangamia

Tangazo lililochapishwa  katika jarida la serikali nchini Zimbabwe limetoa wito kwa mtu yeyote atakeweza kununua wanyama pori wanaopatikana katika  mbuga za wanyama za serikali ajitokeze.


Tangazo hilo  na uamuzi wa kuuzwa kwa wanyama pori nchini Zimbabwe umechukuliwa kutokana na ukame ambao umekumba Zimbambwe.

Emmanuel Fundira ambae ni msimamizi mkuu  wa shirika linalohusika na  safari za watalii
katika mbuga za wanyama amefahamisha kuwa  wanyama ambao wanaathirika ka ukame huo ni punda milia na  tembo.

Ukame huo nchini Zimbabwe umetokana na ukosefu
wa mvua katika maeneo tofauti na kusababisha ukosefu wa maj ina majani.

http://www.trt.net.tr/swahili/afrika/2016/05/08/zimbabwe-yauza-wanyama-pori-kutokana-na-ukame-485712

No comments:

Post a Comment