Na
Kwirinus Mapunda
WILAYA ya Nyasa
mkoani Ruvuma inatarajia kuanza kukimbia kiuchumi baada ya serikali kutoa fedha za ujenzi wa
Barabara ya lami kutoka Mbinga hadi Mbambabay yenye urefu wa takribani kilometa
65.
![]() |
| Mbunge wa jimbo la Nyasa Injinia Stella Manyanya |
Mbunge wa jimbo la
Nyasa ambaye pia ni Naibu waziri wa Elimu, Sayansi,teknolojia na ufundi injinia
Stella Manyanya amesema bajeti ya mwaka wa fedha wa 2016/2017 imeshatenga fedha
kwa ajili ya upembuzi wa kina wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Lituhi
hadi Kitai.
Hata hivyo amesema
bajeti ya wizara ya ujenzi na mawasiliano ya mwaka wa fedha
wa 2016/2017 tayari
zimetengwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa
kilometa kumi toka Kitai hadi Lituhi.
Kaimu meneja wa
TANROADS mkoa wa Ruvuma Laizeck
Alinanuswe amesema serikali imepanga kujenga barabara kwa kiwango cha lami
kutoka Chiwindi-Mbambabay hadi Lituhi ambapo mshauri elekezi anatarajia kuanza
kazi ya upimaji kwa ajili ya matayarisho.
![]() |
| Kaimu meneja wa TANROAD mkoa wa Ruvuma Laizeki Alinanuswe |
“Barabara kwa kiwango
cha lami barabara ya Mpapa-Liparamba-Mipotopoto hadi Mitomoni,barua
ilishaandikwa wizara ya ujenzi,uchukuzi na mawasiliano kwa ajili ya kuhakikisha
barabara hiyo inajengwa’’,alisema.
Kwa mujibu wa kaimu
meneja huyo wa TANROAD bajeti ya mwaka ujao wa fedha imetenga fedha kwa ajili
ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Likuyufusi hadi Mitomoni.
Katika hatua nyingine
ambazo zinaweza kufungua mawasiliano wilayani Nyasa na kuifanya wilaya hiyo
kuanza kukimbia kiuchumi ni ujenzi wa reli itakayoanzia Mtwara hadi Mbambabay
wilayani Nyasa.
Mbunge wa jimbo la
Nyasa injinia Stella Manyanya amesema tayari serikali imepitisha mpango wa
ujenzi wa reli hiyo hivyo amewaasa wakazi wa jimbo hilo kujitayarisha ili
waweze kukuza uchumi wao kuanza ngazi ya familia.
Kuhusu ujenzi wa
daraja la mto Ruhuhu ambalo litaunganisha wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma na
wilaya ya Ludewa mkoani Njombe,injinia Manyanya amesema fedha ya kuanza ujenzi
imetengwa katika bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Alisema kukamilika
kwa ujenzi wa daraja la mto Ruhuhu litaimarisha mawasiliano baina ya wilaya hizo hali ambayo itasaidia
kuimarisha uchumi wa wananchi hasa katika kilimo, usafirishaji na uvuvi.
Kwa miaka mingi
wakazi wa Nyasa na Ludewa wamekuwa wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kuvuka
mto Ruhuhu kwa mitumbwi kutokana na kivuko kutofanyakazi kwa kipindi kirefu
hali iliyosababisha baadhi ya watu kufa maji katika mto Ruhuhu na wengine
wakikamatwa na mamba wakati wanavuka mto huo.
Utafiti umebaini kuwa
kivuko cha Ruhuhu kinafanya kazi kwa miezi mitatu tu kwa mwaka kinaanza mwezi
Juni hadi Agosti,hali hiyo inatokana na serikali kushindwa kujenga gati bora
kwa ajili ya kuweka nanga kivuko kinapotoka upande mmoja wa mto na kwenda
upande mwingine.
Magari yanashindwa
kuvushwa katika kivuko hicho hali ambayo inasababisha kuzunguka kutoka Lituhi,
Songea hadi Njombe kisha Ludewa mjini safari ambayo inachukua siku nzima wakati
kwa kutumia kivuko cha M.V Ruhuhu ni
mwendo wa saa moja hadi Ludewa mjini.
![]() |
| Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nyasa |
Baadhi ya wakazi wa
Lituhi na Ludewa walisema kivuko cha Ruhuhu ni kero ya muda mrefu ambayo hata
Rais mstaafu Jakaya Kikwete anaifahamu na aliahidi kuitafutia ufumbuzi wa
kudumu kwa kuwa inagharimu maisha ya watu kila mwaka pia inazorotesha maendeleo
yao kiuchumi.
Julius Challe
mwenyekiti wa kitongoji cha Lituhi anasema wakazi wa Lituhi wanapata matatizo
makubwa kutokana na ukosefu wa huduma za kivuko cha Ruhuhu hawajui lini tatizo
hilo litapatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa ni tatizo la muda mrefu ambalo
serikali imekuwa itoa ahadi zisizotekelezeka za kujenga daraja.
Wananchi
wanaotegemea kivuko hicho kwa kiwango kikubwa ni kutoka vijiji vya
Msungu,Ilela,Mbongo,Manda,Lupingu na Ngerenge wilayani Ludewa mkoani Njombe na
vijiji vya Lituhi, Nkaya,
Mwelampya,Kihulu,Litumbakuhamba na Ngingama wilayani Nyasa mkoani Ruvuma.
Serikali
iliamua kununua kivuko cha Mv Ruhuhu kama suluhisho la muda wakati ikiendelea
na mikakati ya kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja ambalo litawahakikishia usafiri wananchi
wanaoishi katika maeneo hayo.
Akizungumzia kuhusu
uimarishaji wa bandari na usafirishaji wa meli katika ziwa Nyasa kutoka bandari
ya Itungi kupitia bandari za mwambao mwa ziwa Nyasa zikiwemo
Manda,Ndumbi,Mkili,Liuli hadi Mbambabay injinia Manyanya alisema kazi ya ujenzi
wa meli mpya katika bandari ya Itungi.
“Nilitembelea Itungi
port Kyela ili kufanya
ukaguzi,nimeshuhudia Gati limekamilika na ujenzi wa meli mbili za mizigo tani
1000 kila moja na meli ya abiria unaendelea na bandari ya Ndumbi imeanza
kujengwa’’,alisisitiza.
Kukamilika kwa
miundombinu ya barabara katikakiwango cha lami na ujenzi wa daraja la
Ruhuhu,reli pamoja na kukamilika kwa ujenzi wa meli mpya kusaidia kuimarisha
sekta ya usafirishaji katika wilaya ya Nyasa hali ambayo pia itasababisha
wilaya ya Nyasa kuanza kukimbia kiuchumi.
kwirinusmapunda@yahoo.com



No comments:
Post a Comment