Wednesday, June 29, 2016

Gesi ya Helium yagundulika Tanzania

Zimegundulika futi bilioni 54 za gesi ya Helium

Tanzania inaendelea kupata neema ya rasilimali adimu baada ya  Hifadhi kubwa zaidi ya gesi ya Helium imegunduliwa  katika bonde la ufa la Tanzania.


Hadi sasa Tanzania tayari ina futi za ujazo zaidi ya trilioni 57 za gesi asilia ambazo zimegunduliwa kwa kiwango kikubwa katika mikoa ya Lindi na  Mtwara.

Watafiti kutoka Uingereza wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania
hali ambayo inaweza kubadilisha uchumi wa Taifa na kuifanya nchi kuwa miongoni mwa nchi zenye uchumi wa kati.


Kwa mujibu wa ripoti ya idhaa ya Kiswahili ya BBC ya Juni 28,2016,Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalum wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.

Katika taarifa kwa wanahabri huko Japan, watafiti hao wanasema kuwa uhaba wa gesi hiyo kote duniani ulikuwa umesababisha taharuki haswa kwa madaktari ambao wanatumia gesi hiyo adimu kuendesha mashine za utabibu zijulikanazo kama MRI scanners, mbali na kutumika katika mitambo ya kinyuklia miongoni mwa sekta zingine nyingi za kawi na teknolojia.

Kabla ugunduzi huo watafiti walikuwa wamebashiri ukosefu wa gesi hiyo baridi ifikapo mwaka wa 2035.Mnamo mwaka wa 2010 Mwanfisikia mshindi wa tuzo la Nobel Robert Richardson alikuwa ametabiri kumalizika kabisa kwa gesi hiyo.

Ukosefu huo ulikuwa umesababisha wataalam kuhimiza kutungwa kwa sheria itakayopunguza matumizi yake katika bidhaa zisizo za dharura kama vile kwenye vibofu kutokana na hali ya kuwa gesi hiyo ya Helium ni nyepesi kuliko ile ya Oxygen.

''Gesi tuliyoipata huko Tanzania inaweza kujaza silinda za gesi milioni moja nukta mbili za mashine za MRI'' alisema Chris Ballentine kutoka chuo kikuu cha Oxford.

Mwisho

No comments:

Post a Comment