Wednesday, June 29, 2016

Manispaa ya Songea ina ziada ya madawati 360

Bado madawati 199 katika  shule za msingi,Julai 10 yatakamilika yote


HALMASHAURI ya manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ina ziada ya madawati 360 katika shule za sekondari  hadi kufikia Juni 28 mwaka huu.


Taarifa  ya uwepo wa madawati iliyotolewa jana na  mkurugenzi wa manispaa  hiyo Jenifa Omolo  inaonesha kuwa  madawati (viti na meza) kwa ajili ya wanafunzi wa shule za sekondari  yamekamilika na kuna ziada ya madawati.

Kwa mujibu wa Omolo mahitaji ya madawati katika shule za sekondari yalikuwa ni 10,452,yaliokuwepo ni 9,960,madawati mapya ni 852,yaliopo sasa ni madawati 10,812 na kwamba kuna ziada ya madawati 360.


Hata hivyo amesema taarifa ya madawati katika  shule za msingi katika manispaa hiyo zenye  jumla ya wanafunzi  47,348,mahitaji ya madawati ni 15,783,yaliokuwepo awali ni 9759,yaliotengenezwa ni 5825,madawati yaliopo hivi sasa ni 15,584 na kuna upungufu wa madawati 199 hadi kufikia Juni 28 mwaka huu.

“Madawati 199  yanaendelea kutengenezwa katika karakana ya manispaa ya Songea,yanatarajiwa kukamilika Julai 10,2016’’, imesema taarifa ya mkurugenzi wa manispaa ya Songea.

Afisa habari wa manispaa ya Songea Albano Midelo amesema Mradi wa madawati katika manispaa hiyo ulianza tangu mwezi wa Desemba mwaka 2015  ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania iliyowataka  Wakuu wa Mkoa,Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuhakikisha kuwa hakuna wanafunzi wanaokaa chini hadi kufikia Juni 30 mwaka huu.

Mwisho

No comments:

Post a Comment