Na
Albano Midelo
Serikali ya awamu ya
tano inayoongozwa na Rais John Magufuli imehairisha ajira zote kwa muda hadi
hapo itakapokamilisha kazi ya uhakiki wa watumishi hewa pamoja na kuwaondoa
katika mfumo wa mishahara.
![]() |
| Katibu mkuu Utumishi Dk.Laurean Ndumbaro |
Katibu mkuu utumishi
Dk.Laurean Ndumbaro akizungumza na watumishi wa umma wa wilaya ya Songea kwenye ukumbi
wa manispaa ya Songea amesema zoezi la
kuwaondoa watumishi hewa likimalizika taratibu nyingine za utumishi zikiwemo za
kupanda madaraja na kutoa ajira mpya zitaendelea.
“Ajira mpya na
marekebisho ya mishahara kwa watumishi wa umma havijasitishwa,vimehairishwa (postponed)
kwa muda hadi hapo
uhakiki wa kuwaondoa watumishi hewa utakapokamilika ajira na upandishwaji vyeo kwa watumishi wa umma utaendelea kama kawaida’’,alisisitiza Dk Ndumbaro.
uhakiki wa kuwaondoa watumishi hewa utakapokamilika ajira na upandishwaji vyeo kwa watumishi wa umma utaendelea kama kawaida’’,alisisitiza Dk Ndumbaro.
Amesema serikali hivi
sasa inaweka taarifa za kila mtumishi wa umma katika hali ya usahihi kabla ya
kuendelea na mazoezi mengine na kwamba serikali pia imetoa waraka wa kupitia
muundo wake mpya wa utumishi ili kuona idara na vitengo vilivyopo iwapo bado
vina haja ya kuendelea kuwepo au kupunguzwa hali itakayoboresha utendaji kazi
na kuleta ufanisi kulingana na kasi ya serikali ya awamu ya tano.
Hata hivyo amesema
serikali haitasita kuwachukulia hatua za kisheria baadhi ya maofisa utumishi ambao watashindwa kufanya kazi zao kwa mujibu
wa sheria hali ambayo inawasababisha usumbufu watumishi wa umma ambao
wanawasimamia katika maeneo yao ya kazi hivyo kuwasababishia kukosa ari ya
kufanyakazi baada ya kukosa stahili zao katika utumishi wa umma.
Amewatoa hofu
watumishi wa umma kwa changamoto ambazo wanazipata katika kipindi hiki cha
mpito na kwamba wizara ya utumishi wa umma ipo tayari kusikiliza changamoto
zinazowakabili watumishi na kuzitafutia ufumbuzi wa kuduma.
Katibu mkuu utumishi
amefanya ziara ya siku mbili mkoani Ruvuma akiwa na watendaji wake wa wizara ikiwa
ni wiki ya utumishi wa umma ambayo inaanza Juni 16 hadi Juni 23 kila mwaka
ikiwa na lengo la kutenga siku moja ya kuwatembelea na kusikiliza kero
mbalimbali za watumishi wa umma na kuzitafutia ufumbuzi.
Baadhi ya watumishi
wa umma wa wilaya ya Songea wamefarijika na ziara hiyo ya katibu mkuu ambapo
wamepata fursa za kutaja changamoto mbalimbali zinazowakabili katika utumishi
wa umma ikiwemo ya kuchelewa kupanda vyeo, kutopata fedha za likizo kwa wakati
na kutorekebishiwa mishahara yao kwa wakati.
Baadhi ya changamoto
zimeweza kushughulikiwa na katibu mkuu papo hapo kwa kushirikiana na timu yake
yote kutoka wizarani jambo ambalo limepongezwa na watumishi wa umma ambao
baadhi ya wamehaingaika kwa kati ya miezi sita hadi miaka mitatu bila ufumbuzi.
![]() |
| Baadhi ya watumishi wa umma wa Songea mjini |
Awali mkurugenzi wa
manispaa ya Songea Jenifer Omolo akizungumza na watumishi wa umma wa manispaa
hiyo katika wiki ya utumishi wa umma amewakumbusha kufanyakazi kwa misingi ya
utumishi wa umma.
“Hata kama unakunywa
kunywa kama mtumishi wa umma badala ya kuwa mlevi,kuanzia sasa watumishi wote
wa umma ambao watakwenda kinywe cha maadili wataitwa katika vikao vya
maadili,kama wewe ni mlevi tutatumia evidence ikiwemo kupigwa picha wakati
umelewa tafadhali naomba kila kitu mfanye kama watumishi wa umma’’,alisisitiza.
Mwisho.


No comments:
Post a Comment