Mwenge wa uhuru katika manispaa ya Songea umefanikiwa kufungua miradi sita katika maeneo mbalimbali ya manispaa ya Songea ukiwemo mradi wa madawati 100 katika shule ya msingi Luhira,kupandamiti chanzo cha maji ya SOUWASA,kufungua stendi ya mabasi ya Songea mjini,uzinduzi wa nyumba ya mkurugenzi wa manispaa ya Songea,madarasa mawili katika shule ya sekondari Chabruma na mradi wa ng'ombe wa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI katika eneo la mwenge mshindo.
Mwenge wa uhuru katika manispaa ya Songea umeweza kufanya miradi hiyo yote kwa amani na usalama ambapo katika miradi hiyo yote mamia ya wakazi wa manispaa ya Songea walijitokeza kwa wingi ikiwa ni pamoja na kukesha hadi asubuhi,wakishangilia na kucheza hata baada ya mwenge kuondoka katika eneo la mkesha katika shule ya Kibulang'oma.
Mwenge wa uhuru ulimaliza salama mbio zake katika manispaa ya Songea na Juni 9 mwaka huu ulikabidhiwa katika Halmashauri ya Mbinga.![]() |
| Mwenge wa uhuru ukiwa mpakani mwa wilaya ya Namtumbo na Songea katika kijiji cha Shule ya Tanga |
![]() |
| Katibu tawala wa wilaya ya Songea akisoma risala ya utii kwa Rais katika majumuisho ya mbio za mwenge kitaifa manispaa ya Songea kwenye viwanja vya kibulang'oma |
![]() |
| Mradi wa madarsa mawili katika shule ya sekondari Chaburuma manispaa ya Songea ambayo yalifunguliwa na Mwenge |
![]() |
| Mwenge wa uhuru ukiwa unaingia katika stendi ya mabasi ya mjini Songea kwa ajili ya uzunduzi wa stendi hiyo |
![]() |
| Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa 2016 akiwa ndani ya stendi ya mabasi ya Songea baada ya kufanya uzinduzi |
![]() |
| Viongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa wakiwa Songea TTC |
![]() |
| Madawa ya kulevya ambayo yalikamatwa na polisi yakichomwa siku ya mbio za mwenge kitaifa 2016 shule ya msingi Mloweka |
![]() |
| Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa akiwa na mkuu wa wilaya ya Songea pamoja na mkurugenzi wa manispaa ya Songea katika chanzo cha maji cha SOUWASA ambako ilifanyika kazi ya upandaji miti kitaifa |
![]() |
| Mbio za mwenge wa uhuru stendi ya mbasi Songea |
![]() |
| Wanakwaya wa Songea TTC wakitumbuiza siku ya mwenge |
![]() |
| Vijana wadogo wakitumbuiza siku ya mapokezi ya mwenge wa uhuru kitaifa |
![]() |
| Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa akipanda mti katika chanzo cha Ruhila |
![]() |
| Kikundi cha ngoma ya mganda katika kijiji cha Mwengemshindo wakitumbuiza siku ya mwenge |
![]() |
| Mwenge wa uhuru ukiwa katika kijiji cha Mwengemshindo Songea mjini |
![]() |
| Add caption |


















No comments:
Post a Comment