Na Julius Konala
Ukaguzi wa usafi na mazingira katika majengo na nyumba uliofanyika katika
manispaa ya Songea mkoani Ruvuma umebaini kuwa asilimia zaidi ya 92 ya nyumba
katika manispaa hiyo zilikuwa bora.
Ofisa habari wa
Manispaa ya Songea
Albano Midelo alisema kuwa manispaa hiyo
ilifanya ukaguzi wa usafi wa
Mazingira katika nyumba 2,674.
Kwa ajili ya kufuatilia usafi wa mazingira, ujenzi wa nyumba,vyoo bora, matumizi ya vyandarua, utunzaji wa maji katika Kaya pamoja
na visima vya maji majumbani.Kwa ajili ya kufuatilia usafi wa mazingira, ujenzi wa nyumba,vyoo bora, matumizi ya vyandarua, utunzaji wa maji katika Kaya pamoja
“Lengo lilikuwa kukagua nyumba 2588 hata hivyo hadi
kufikia Desemba 2015 nyumba 2565 zilikaguliwa sawa na asilimia 99.6, katika
ukaguzi huo nyumba 2396 zilikuwa bora sawa na asilimia 92.90’’,alisema.
Katika kutekeleza agizo la Rais
Dr.John Magufuli la kufanya usafi wa
mazingira Halmashauri ya Manispaa ya Songea imekuwa kila Jumamosi ya mwisho wa
mwezi inafanya shughuli mbalimbali za usafi katika kata zote 21 na mitaa 95
inayounda manispaa hiyo.
Kwa mujibu wa Midelo kazi za usafi wa
mazingira ambazo zimekuwa zinafanywa ni pamoja na Kufagia, kukusanya takataka na kuzizoa kwenye
maeneo ya makazi, biashara na Taasisi, kulima na kufyeka nyasi, kufukua
mifereji ya maji ya mvua na kufukia mashimo na madimbwi.
Ili kuhakikisha kuwa wananchi
wanajengewa uwezo katika suala la utunzaji na usafi wa mazingira,Idara ya afya
na mazingira inawaelimisha wananchi kuyaweka mazingira katika hali ya usafi
kupitia vyombo vya habari pamoja na kutumia gari lenye kipaza sauti.
Takwimu zinaonesha kuwa mwezi Desemba
2015 pekee katika manispaa ya Songea, tani zaidi ya 303 za taka ngumu
zilikusanywa na kwamba tani zilizopelekwa dampo zilikuwa tani 194.
Amesema operesheni ya usafi wa
mazingira kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi imekuwa inafanywa na wakazi wote
katika manispaa hiyo wakiwemo Majeshi,Watumishi
wa Umma, Taasisi za Umma, Taasisi binafsi,Mashirika ya Umma, Asasi za kidini na
asasi za kiraia.
Ili kukabiliana na wachafuzi wa
mazingira,amesema,mashtaka na faini za papo kwa papo zimekuwa zinatolewa
kutokana na faini za uvunjaji wa sheria mbalimbali za Afya na usafi wa
mazingira,lengo likiwa ni kuuweka mji wa Songea katika hali ya usafi.
Pia
kunafanyika Ukaguzi wa vyakula mbalimbali ili kutambua iwapo vina vifaa kwa
matumizi ya binadamu na kwamba vyakula ambavyo havistahili vinaondolewa ambapo tayari vyakula na vinywaji ambavyo
havifai kwa matumizi ya binadamu vyenye thamani
ya zaidi shilingi milioni tano.
Hata hivyo amesema Elimu ya afya juu
ya matumizi ya maji safi na salama inaendelea kutolewa kwa njia ya vyombo vya
habari na mikutano ya hadhara ili kuepukana na magonjwa mbalimbali ya mlipuko.
MWISHO
No comments:
Post a Comment